Ijumaa, 24 Novemba 2017

NAMNA YA KUWASILIANA NA WATOTO VIZIWI



Watu wengi wanashindwa kuwasiliana na watoto viziwi kwa kufikiri kwamba lazima awepo mkalimani wa lugha ya alama au Mwalimu wa viziwi ndiyo watu pekee wa kuweza kuwasiliana nao jambo ambalo siyo sahihi.Mambo yafuatayo ukiyazingatia kwa ukamilifu yatakusaidai kuweza kuwasiliana na watoto viziwi;

1.       Hakikisha kwamba unateka makini ya mtoto kabla hujaanza kuongea naye.Jaribu kumpungia mkono au kumgusa kidogo begani.(usimrushie jiwe,usimwite kwa kumpigia makofi)

2.     Mtizame yule mtoto ana kwa ana unapoongea naye.Kila mara hakikisha kuwa mtoto huyo anaweza kuuona uso wako vyema.Ikibidi keti au chuchumaa ili uso wake uwe sambamba na wako.

3.     Tumia vitu vinavyoonekana iwezekanavyo.Ashiria kwa mkono kitu au kifaa unachozungumzia.

4.      Mweleze mtoto mada unayozungumza au mjulishe unapobadilisha mada.

5.      Simama uso wako ukitizama kwenye mwangaza.

6.       Jaribu kumwambia arudie kile au yale uliyoyasema iwapo huna hakika kama amekuelewa.

7.   Mra nyingi mazungumzo ya vikundi yanaweza kuwa magumu kwa mtoto kiziwi.Mshirikishe kila hatua.Hakikisha kuwa wanazungumza kwa zamu.

Zingatia:Ongea kwa njia ya wazi na jaribu kuonesha hisia usoni kwa kile unachozungumza

Maoni 2 :

  1. Asante kwa uelimishaji tutazingatia yote ili tuweze kufanikisha malengo waliyinayo watoto Hawa wenye mahitaji maalum

    JibuFuta