Lugha
ya alama ni lugha ya ishara inayotumiwa na jamii ya viziwi katika kufikisha
ujumbe unaokusudiwa kwa muhusika.Lugha hii utumia viungo vya mwili ili iweze
kufanya kazi,viungo hivyo ni mikono,vidole,kichwa,macho,kiwiliwili,masikio,mdomo,ulimi
na pua.
Kwa
mujibu wa watu wenye uziwi,kuna lugha ya alama ya Asili na lugha ya alama Rasmi.Lugha
ya alama ya asili ni lugha ya alama inayotumiwa na baadhi ya viziwi katika eneo
dogo la jiografia wakati lugha ya alama rasmi ni lugha iliyosanifiwa na
inatumiwa na idadi kubwa ya viziwi.
Kiziwi
ni mtu yoyote mwenye matatizo ya kusikia au asiyesikia kabisa.Tunaposema kwamba
mwenye matatizo ya kusikia tunamaanisha ni wale watu wanaosikia kwa shida au
usikivu wao ni wa majira (Hard of hearing) ila asiyesikia kabisa ni mtu ambaye
hawezi kutafsiri sauti ya kitu au kutambua sauti.Kuna viwango tofauti tofauti
vya usikivu.
Kutokana
na mabadiliko ya kisayansi na kimazingira idadi ya viziwi inazidi kuongezeka
ulimwenguni kote hivyo kupelekea kuongezeka kwa mahitaji ya lazima (kuwa na
shule za viziwi,walimu maalum,wakalimani,vifaa vya usikivu,mawasiliano(Lugha ya
alama),sera itakayowalinda dhidi ya makundi mengine) ili waweze kukidhi haja
zao za kila siku.Mabadiliko ya kisayansi na kimazingira yanayochangia
kuongezeka kwa idadi ya viziwi ni matumizi ya mabomu,magonjwa kama vile
magonjwa ya zinaa kwa mama wajawazito,matumizi mabaya ya madawa makali (quinine),uti
wa mgongo,uvutaji wa bangi kwa mama wajawazito, makelele viwandani na umri
mkubwa kuanzia miaka 64 kuendelea nk Lakini si watu wote wanaopata uziwi
wanajikubali na kujitokeza katika jamii
Hadi
sasa hakuna idadi kamili ya viziwi nchini Tanzania kutokana na ugumu wa kuwatambua
viziwi. Serikali haijaweka kipengele
maalum kwenye karatasi za sensa ili kama familia hina mtu mwenye uziwi aweze
kuhesabiwa katika kipengele maalum pia familia nyingi zinakosa uelewa hivyo
kupelekea kuwaficha watoto wenye uziwi ili kukwepa aibu mbele ya jamii wakati
mwingine viziwi wenyewe huwa hawajikubali kabisa kama wao ni viziwi hivyo ni
vigumu sana kutambua idadi kamili ya watu wenye uziwi nchini Tanzania.
Hivyo
kama walivyo binadamu wengine wanavyowasiliana na jamii moja na nyingine ili
kufanikisha shughuli zao kwa ufanisi basi viziwi nao wanahitaji lugha ya alama
ili waweze kufanikisha shughuli zao za kila siku bila ya hivyo inawawia vigumu
sana.Kitu cha kuzingatia ni kwamba suala la ugumu wa mawasiliano kwa viziwi ni
jambo linalomgusa kila mtu moja kwa moja bila kujali kama wewe ni kiziwi au si
kiziwi.Iwapo kama viziwi watasikilizwa na lugha ya alama kupewa kipaumbele
katika matumizi ya kila siku kutakuwa na manufaa haya:
Kuweza
kupata ujumbe unaozungumzwa kwa haraka na wakati sahihi,Mara nyingi viziwi ni
kundi la mwisho kupata habari inayozungumzwa katika jamii kutokana na hali yao
hivyo kuhatarisha maisha yao au kuwafanya kuwa nyuma kiuelewa hivyo kuonekana
wagumu kuelewa au kwenda na wakati kulingana na kitu kinachozungumzwa sasa
lakini kuna njia wanazotumia baadhi ya viziwi ili waweze kujipatia ujumbe kwa
haraka sasa hivi kuna simu janja ambapo
taarifa zote zinafika kwa wakati kwa njia ya mtandao pia ujiunga katika
mitandao ya kijamii.Ila si wote wenye uwezo wa kununua simu za janja.
Kuweza
kujitegemea wenyewe ,Mawasiliano ni mbinu mojawapo inayomkuza mtoto yoyote yule
kiakili na hata kimaisha hivyo iwapo kama kiziwi atapatiwa mawasiliano sahihi
kutamfanya ajielewe kwa wakati kulingana na umri wake hivyo kuachana na
utegemezi katika wakati mwafaka.
Kupata
elimu katika mazingira bora na wakati sahihi,Hivi sasa viziwi hawapati elimu
iliyo bora na katika mzingira mazuri kitu kinachowakatisha tamaa mapema
sana.Shule nyingi za viziwi, matumizi ya lugha ya alama si ya kulidhisha sana
bali walimu hujikuta wanafundisha ilimradi tu lakini sikumuelewesha mtoto kiziwi.Ni
vizuri jamii ielewe kwamba ukimuacha mtoto kiziwi bila kuelewa chochote ni
kuongeza mzigo katika jamii.
Kuweza
kujikomboa kifikra,Kwa kuwa ni lugha yao wataweza kuelewa kile kinachozungumzwa
hivyo kuweza kujikomboa kifikra.Ukombozi wa fikra ni muhimu sana kwa mwanadamu
yoyote yule bila kuwa na ukombozi wa fikra ni hatari sana kwa maendeleo ya
mtu.lakini iwapo tu lugha ya alama ikapewa kipaumbele kutumika kwenye nyanja
zote sidhani tatizo la ukombozi wa fikra litakuwepo kwa viziwi.
Kufurahia
hali waliyonayo,Kutokana na ugumu wa mawasiliano baina ya viziwi na wasio
viziwi upelekea viziwi wengi kutokuwa na furaha juu ya uziwi wao kwani ujikuta
wakitamani nao wawe kama wengine ili waendane nao katika mawasiliano na
kupatana na kila mtu lakini tu iwapo kama lugha ya alama itapewa kipaumbele kwa
watu wote basi viziwi nao watajisikia watu wenye furaha na kukubali hali
waliyonayo kuliko kujikana kitu ambacho kinaleta usumbufu kwa jamii.
Kupunguza
muda wa kupata taarifa,Siku hizi kiziwi akikamatwa na askari ni lazima apelekwe
shule ya viziwi au kwenye taasisi ya viziwi ili aweze kuhojiwa kitu ambacho ni
fedhea kwake kwani kinamvunjia heshima katika jamii.Kuna sehemu nyingine viziwi
huwa wanatoka majumbani mwao na kusafiri umbali mrefu ili kukutana na wenzao tu
kwa lengo la kupata taarifa matokeo yake ni kupoteza mda ambao angeutumia
katika kufanya kazi zingine muhimupia baadhi ya watu wenye uziwi ulazimika
kutoka majumbani mwao kwenda kujiandikisha au kupiga kura katika shule za
viziwi bila kujali umbali hii yote ni kwasababu ya ugumu wa mawasiliano.
Kuibua
au kukuza vipaji,Ugumu wa mawasiliano ndio unawafanya watu wengi
kutojishughulisha kikamilifu na watu wenye Uziwi katika mambo
mbalimbali.waandaaji wengi wa masuala ya ubunifu au kukuza vipaji hushindwa
kuwasaidia viziwi kwa sababu ya kuwa na wasiwasi na mawasiliano hivyo kama
lugha ya alama itapewa kipaumbele na watu wataichukulia ya kawaida hivyo
hawatasita kuwasaidia watu wenye uziwi nchini.
UMUHIMU
WA LUGHA YA ALAMA KWA JAMII
•Kurahisisha
mawasiliano na Viziwi
•Ajira
kwa wakalimani
•Mawasiliano
ya siri (inaweza kutumiwa bila watu kujielewa kama wanazungumzwa wao)
•Kitambulisho
cha utamaduni wa viziwi wa Tanzania
•Kuburudisha
jamii kupitia vionjo vya lugha ya alama
Ni
vizuri jamii ikaungalia Uziwi kwa jicho la pili ili kuweza kuwasaidia kutimiza
mahitaji yao.ikumbukwe kwamba nawe siku moja utaweza kuingia katika kundi hili.
Shabani kahaya
0719999861
Whatsapp
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni